Wednesday, February 4, 2009

wanajeshi, polisi, raia watwangana

juzi Februari 2, majira ya saa 2 usiku katika mji mdogo kulizuka vurugu baina ya Polisi, Wanajeshi na Raia. Chanzo cha vurugu kinadaiwa kuwa ni Askari Polisi kumsimamisha mwendesha Pikipiki ambaye inadaiwa alikuwa hajavaa Helmet na pikipiki ikiwa haina namba. Inadaiwa kuwa katika mahojiano kulitokea kutoelewana na ndipo Mwendesha pikipiki anayedaiwa kuwa ni Mwanajeshi wa kikosi cha Mbalizi alipotaka kuondoka na askari polisi kuiwahi na kuifunga pingu na hatimaye kuzuka vurugu zilizojumuisha makundi matatu, Polisi kwa upande mmoja na Wanajeshi na Wananchi kwa upande mwingine.Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya Zelothe Stephene anasema hawezi kuzungumzia suala hilo kwa kuwa linawahusu askari na litamalizwa kwa taratibu zao. Cha kujiuliza hapa. Kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania hakuna mtu aliye juu ya sheria na kwamba yeyote anayevunja sheria anapaswa kuchukuliwa hatua kali za kisheria. Ndugu zangu Watanzania tunazungumziaje matukio yanayowahusisha wanajeshi kuvunja sheria kwa makusudi na wakihojiwa ni vurugu mtindo mmoja. Je kuna ukweli kuwa wapo juu ya sheria

No comments:

Post a Comment