Kupitia blog hii utapata nafasi ya kuyajua mambo yanayojiri kila siku katika Mkoa wa Mbeya zikiwemo, habari mbalimbali zinazohusu jamii, matukio, na tetesi mbalimbali. Pia kupitia blog hii tutajadili masuala mbalimbali ya maendeleo yanayohusu Mkoa wa Mbeya.
Wednesday, February 4, 2009
wanajeshi, polisi, raia watwangana
juzi Februari 2, majira ya saa 2 usiku katika mji mdogo kulizuka vurugu baina ya Polisi, Wanajeshi na Raia. Chanzo cha vurugu kinadaiwa kuwa ni Askari Polisi kumsimamisha mwendesha Pikipiki ambaye inadaiwa alikuwa hajavaa Helmet na pikipiki ikiwa haina namba.
Inadaiwa kuwa katika mahojiano kulitokea kutoelewana na ndipo Mwendesha pikipiki anayedaiwa kuwa ni Mwanajeshi wa kikosi cha Mbalizi alipotaka kuondoka na askari polisi kuiwahi na kuifunga pingu na hatimaye kuzuka vurugu zilizojumuisha makundi matatu, Polisi kwa upande mmoja na Wanajeshi na Wananchi kwa upande mwingine.Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya Zelothe Stephene anasema hawezi kuzungumzia suala hilo kwa kuwa linawahusu askari na litamalizwa kwa taratibu zao.
Cha kujiuliza hapa. Kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania hakuna mtu aliye juu ya sheria na kwamba yeyote anayevunja sheria anapaswa kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
Ndugu zangu Watanzania tunazungumziaje matukio yanayowahusisha wanajeshi kuvunja sheria kwa makusudi na wakihojiwa ni vurugu mtindo mmoja. Je kuna ukweli kuwa wapo juu ya sheria
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment