Tuesday, February 24, 2009

Ofisi hii wanaamini Mzee Ruksa bado ni Rais

Mbunge Zitto Kabwe akisisitiza jambo wakati wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za mitaa ilipofanya ziara wilayani Mbozi, nyuma ni Picha ya Rais mstaafu wa awamu ya pili Ally Hassan Mwinyi. badala ya kuweka picha ya JK wenzetu hawa sijui wanaishi dunia gani hawatambui kuwa serikali hii ni ya awamu ya nne.
Mbunge wa Mbarali, Estherina Kilasi akizungumza katika kikao hicho naye ni kama hakuiona picha hiyo ya Mwinyi huku ya Mwenyekiti wa CCM na Rais JK ikiwa haipo.
Huyu yeye aliamua kufumba macho kabisa ili asiione
Hadi leo kuna baadhi ya maeneo nchini wanaamini kuwa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu J.K Nyerere ni Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini kwa walio maofisini yote nchini wanauelewa mpana kwamba Serikali iliyopo Madarakani ya awamu ya nne ikiwa chini ya Rais Jakaya Kikwete.
Kabla ya Kikwete Marais waliopita ni pamoja na J.K Nyerere, All Hassan Mwinyi, Benjami Mkapa na sasa Rais Kikwete. Kwa taratibu zilizopo ukiingia katika ofisi nyingi hapa nchini, utakuta kuna picha ya Rais wa awamu ya kwanza na aliyepo madarakani kwa wakati.

No comments:

Post a Comment