Tuesday, November 16, 2010

Breaking News

Mizengo Peter Pinda ndiye waziri mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mwaka 2010-2015, mtoto wa mkulima kutoka katika jimbo la Katavi Mkoa mpya wa Katavi.

Monday, November 8, 2010

Breaking news

Haile Gebrselassie(37) rasmi amejiuzulu katika mbio za marathon baada ya mguu wake kupata hitilafu katika mbio za marathon New York, anasema anafikiria kuingia katika siasa lakini kabla ataangalia namna ya kuwasaidia wananchi wa Ethiopia. mfukuza upepo huyo anamiliki shule mbili, ni wakala wa kuuza magari, hoteli na biashara kadhaa ambazo zimetoa ajira kwa Raia wa Ethiopia

Wednesday, October 27, 2010

Pweza Paul

Pweza Paul afariki

Pweza Paul aliyeondokea kuwa mtabiri maarufu katika michuano ya Kombe la dunia 2010, amefariki. Paul amefariki kifo cha kawaida, ambapo kwa mujibu wa wataalam, Pweza huishi kwa wastani wa miaka miwili na nusu na Pweza Paul alikuwa tayari katika umri umri

Tuesday, October 19, 2010

Siasa

Ni kama anasema 'tatizo lenu hamnielewi nyie waandishi sijasema hilo, oo nasinzia kwa msisitizo

Monday, October 18, 2010

Siasa

Nani anasema eti tunabebwa na malori kwenda kwenye kampeni?sie tunasafari zetu kwani kuvaa sare imekuwa kosa?ndivyo wanavyoelekea kusema

Thursday, October 14, 2010

Mama na mtoto

Aaaa nimeyaona magimbi ngoja nimuwahi anayeuza hata mososi wa hapa restaurant siutaki tena, ni kama anavyoelekea kusema kijana anayetoka restaurant. magimbi kwa chai usipime

Wednesday, October 13, 2010

Vijana

Haa unadhani ntakusaidia, najifanya niko busy naangalia pembeni, nani kakwambia uzidishe mzigo"ni kama anasema mpitanjia.

Tuesday, October 12, 2010

Uwindaji

aaaa maisha ya vijijini kwetu raha mustarehe, hakuna haja ya kupanga foleni kwenye butcher, aa sie twawinda ndege enzi hizo tunaita vinjuni, huku kwetu lakini sijui kijijini kwenu, "aaa simkosi huyo lazima nimdungue"

Monday, October 11, 2010

Kwa taarifa yako

Enzi hizo, nakumbuka sarakasi tulikuwa tunaangalia mashuleni wakija wanne star na wenzake, sie tulikuwa tukimwita wane, lakini kwa sasa mchezo huo si maarufu ingawa si maarufu.

Mitaani kwetu

Mchezo wenyewe ulianza hivi, aisee mi ntakutoa ngeu hivi hunifahamu eee?????
Haa yaani tumevua mashati nakukimbia lakini bado unakuja?hivi unadhani sikuogopi nitakutoa meno ohoo
aaaaa nyie mtauana achanen, mnajifanya wajanja wee muachie mwenzako utamuua.
Kama Kenya wengine wanatazama sinema ya bure tena masumbwi kavu kavu ambayo ni adimu huku wengine wakisonga na shughuli zao kama kawa.

Monday, September 27, 2010

ajali ya mwenyekiti

Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya,(MBPC), Nico Mwaibale pamoja na mkewe pamoja na Katibu Mkuu wa MBPC, Patrick Kossim na abiria mwingine ambaye hajafahamika jana walinusurika kufa baada ya gari yao kupata pancha tairi la nyuma, katika eneo mafinga na gari yao kutumbukia kolongoni , lakini wote ni wazima, gari imetolewa korongoni linarudishwa Mbeya kwa matengenezo na majira ya saa 10 hivi walikuwa wanajiandaa na safari ya kuelekea DSM, sasa kwa basi na si kwa gari binafsi tena

Saturday, May 22, 2010

Hawa nao ni watoto wa Kitanzania

Hawa nao ni watoto wa Kitanzania waliopo Iganjo uyole Jijini Mbeya, watoto hawa nao wapo Tanzania na ni watanzania, hapa walikuwa wametoka kuogelea katika mto na kukutana na baadhi ya waandishi waliokuwa wametembelea mradi wa umwagiliaji wa Iganjo.
Mwandishi wa Baraka FM ya Jiji Mbeya akizungumza na mmoja wa watoto huku mwenzake akifanyajitihada za kuhakikisha suruali yake isimdondoke.Uwezeshaji kiuchumi wananchi utasaidia kuboresha maisha sawa kwa watoto wote na wao kuweza kumudu kusoma katika shule bora,kuishi maisha bora kama ilivyo kwa watoto wengine.

Friday, May 21, 2010

Tutapona kweli

Wakulima wa Bonde la Uyole wakisafisha karoti katika mto ulio karibu na daraja la Igawilo nje kidogo ya Jiji la Mbeya.Baadhi ya watu wanatabia ya kula karoti zikiwa hazijaoshwa mara baada tu ya kununua kutoka sokoni. Ofisi ya Mkemia Mkuu imefunguliwa Mbeya ni nafasi ya ofisi hiyo kuchunguza kama maji hayo yanafaa kwa matumizi ya binadamu.

Thursday, May 20, 2010

Kilimo Kwanza na waandishi

Wakulima wa Iganjo wakiwa wanapanda viazi.Uyole ni moja ya eneo linaloongoza kwa uzalishaji wa viazi,nyanya, vitunguu na mahindi, ambapo eneo hilo linategemea zaidi kilimo cha umwagiliaji.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa wanamuhoji mmoja wa wakulima katika mashamba ya umwagiliaji ya Iganjo.

Wednesday, May 19, 2010

Ofisi ya Mkemia Mkuu sasa Nyanda za Juu Kusini

Kwa wale wenye tabia ya kupachika mimba wanafunzi, wanaokataa au kusingiziwa watoto, kubaini wanaohusika na mauaji ya watoto na uchunaji ngozi pamoja na uchunguzi wa kisayansi kama kwa maji ya kisima na mengine. Sawa dawa ipo sebuleni na si jikoni tena Baada ya Mkemia Mkuu kufungua ofisi kwa Mikoa ya Nyanda za Juu kusini. Wananchi tutumie fursa hii kwa ajili ya utatuzi wa mambo mbalimbali yanahusiana na tafiti za kisayansi.Tuelewe kuwa ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali si kwa ajili ya kushughulikia masuala ya jinai tu

Monday, May 17, 2010

Siku ya familia Duniani

Jumamosi, May 15, nilibahatika kuhudhuria maadhimisho ya siku ya familia Duniani ambayo Jijini Mbeya yaliazimishwa katika viwanja vya shule ya msingi Nzovwe, kwa umuhimu wa siku yenyewe iliyoandaliwa na taasisi ya Champion nilitaraji wazazi wangehudhuria kwa wingi, lakini idadi ya watoto ilikuwa kubwa huku matumizi ya kondomu yakihimizwa
Picha ya juu ni baadhi ya vijana walioshiriki katika maadhimisho ya siku hiyo wakiwa na kondomu za familia walizogawiwa, na chini baadhi ya watoto waliokuwa wamejazana katika uwanja huo

Sunday, March 21, 2010

Mmmh Miss wetu

Huyu ndiyo Miss Mbeya 2009, Marry akipata burudani ya mpira wa pete na watoto wa kituo cha yatima mbalizi, chini akikabidhi zawadi

Saturday, March 20, 2010

usafiri wetu

Hii ndio Tanzania bwana, wakati watu wanasafiri na magari ya kifahari ikiwemo VX, Lexus na mengine unayoyajua, Hii ni chunya na huo ndio usafiri wenyewe.
Ndio Maisha yenyewe haya

Saturday, March 6, 2010

Mama na Mtoto

Ukistaajabu ya Musa utayaona ya filauni, ni huko Cambridge, Uingereza
Mtoto Xavier King (pichani) aliwaacha watu vinywa wazi baada ya kuanza kutembea bila kutambaa tofauti na hatua za ukuaji wa kawaida wa mtoto. Mtoto huyo ambaye Februari 15, mwaka huu alitimiza miezi sita, alinyanyuka ghafla wiki moja kabla ya siku hiyo na kutembea akiwa ameshika ukuta. Hiyo ilikuwa hatua yake ya kwanza ya kuanza kutembea bila msaada wowote. Hatua hiyo haikuwashangaza sana wazazi wake, kwani waliamini kwamba alikuwa akicheza, ikizingatiwa kuwa mara kwa mara alikuwa akianguka. Siku mbili baadaye, mtoto huyo alianza kutembea bila kushika popote., mara hiyo akifanya hivyo kwa umbali wa futi sita kutoka mahali anapokuwa. Hapo ndipo alipowashangaza wazazi wake. “Sikuwa na mawazo hayo na kamwe sikuwahi kufikiria jambo la ajabu la aina hiyo. Kama mzazi niliishia kushangaa, nilimpigia simu baba yake kazini na kumwabia, naye alishangaa, “ anasema mama wa mtoto huyo, Mary King (30). Mzazi huyo ambaye ni muuguzi anasema, watoto wengi huweza kutembea baada ya kufikisha miezi 10 ama mwaka mmoja.

Sunday, February 28, 2010

Kwa Taarifa yako

Siku mtu mfupi duniani na mtu mrefu walipokutana