Tuesday, February 24, 2009

Eti polisi kampiga kijana risasi bila sababu?

Kuna tetesi zimeenea kuwa askari polisi mmoja amemjeruhi kijana mmoja mkazi wa mabatini kwa kumpiga risasi ya mguuni kwa kile kinachodaiwa eti ni bahati mbaya. tetesi zaidi zinadai kijana huyo alilazwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya na kuruhusiwa kutoka Februari 23, baada ya madaktari kubaini kuwa risasi hiyo ilipita kwenye mnofu na haikugusa mfupa. Kinachosemekana sasa ni kuwa huyo askari aliyemjeruhi kijana huyo alitoa kwa siku mbili tu na kisha akaingia mitini. Wadau fuatilieni ili tupate ukweli wa tetesi hizi kama ni za kweli

No comments:

Post a Comment