Friday, February 6, 2009

Prison yaona mwezi

Baada ya kupata vipigo mfululizo, jana timu ya Tanzania Prison iliona Mwezi kwa kuichapa timu ya Mtibwa sugar goli 2-1. Wakati iliwachukua Mtibwa dakika 13 kujipatia goli la kwanza, Prison walilazimika kusubiri hadi dakika ya 75 na 84 pale Laurian Mpalila na Ismail Suleima (zamani akijulina kama Suma Addo) walipoweza kupachika magoli maridadi na kumwacha kipa Shaban Hassan 'Kado' na wenzake wakishika vichwa kwa mshangao. hata hivyo kwa mujibu wa wachambuzi wa soka timu hiyo iliyopteza Mechi nne mfululizo bado ina kazi ya ziada ili iweze kufanya vizuri. Ilianza mzunguko wa pili kwa kuchapwa goli 2-0 na Villa Squard, ikachapwa 3-1 na Simba, ikaburuzwa goli 1-0 na Yanga katika Uwanja wa kumbuklumbu ya Sokoine kabla ya kuchapwa goli 2-0 na Walibya katika Michuano ya Kimataifa. Inashika nafasi ya nne ikiwa na pointi 22.

No comments:

Post a Comment