Wednesday, February 12, 2014

Wasomi watakiwa kutotumia jazba kujadili masuala ya muungano

Na Merali Chawe, Mbeya

Wasomi nchini wametakiwa kujadili hoja za muungano kwa umakini na busara na waepuke jazba ambazo hazina maslahi kwa Taifa.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro aliyasema hayo alipokuwa akifungua Kongamano la wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu vilivyopo Mkoani hapa lillojadili tathmini ya miaka 50 ya utekelezaji wa masuala ya Muungano.

Alisema wasomi wanatakiwa kujadili hoja za Muungano kwa kuwa makini, wastahmilivu na wawe makini kutoa maoni kwa manufaa makubwa na mustakabali wa Taifa.
Na Merali Chawe , Mbeya

Baadhi ya wakazi Mkoani Mbeya wameuomba uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kuwajengea jengo la kupumzikia wakati wakisubiri kuwaona wagonjwa wao ili kuepuka adha za mvua na jua kali.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, walisema kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakilazimika kukaa kwenye jua na wakati mwingine kunyeshewa na mvua wakati wakisubiri muda wa kuruhusiwa kuinia kuona wagonjwa wao.