Wakati tukiwa tumeelekeza macho na masikio yetu katika utamaduni wa nchi za kimagharibi kwa kuiga mavazi, utamaduni wao, muziki na hata namna ya kula na kuzungumza na kusahau tamaduni za kwetu hasa katika nyimbo za asili.
Ukifika Mkoani Mbeya hususani katika wilaya ya Mbozi utakumbuka zamani kwa kushuhudia ngoma maridadi za asili na kusahau kabisa mambo ya bongo flava, R&B na miziki ya sebene kutoka kongo na mengineyo huku ukipata vionjo vya asili kuanzia sauti, filimbi hadi midundo ya ngoma.
No comments:
Post a Comment