Tuesday, February 17, 2009

Breaking news

Ama kweli ukishangaa ya Musa utayaona ya filauni.Mchungaji wa Kanisa la Pentecoste lililopo Idiwili kata ya Iyula wilayani Mbozi anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kukutwa na mabaki ya mwili binadamu yanayohisiwa kuwa ni mabaki ya mtu mwenye ulemavu wa ngozi (Albino) waliyokuwa wanayauza kwa zaidi ya shilingi milioni 30. Mchungaji huyo, Cosmas Mwasenga (39) anashikiliwa kwa pamoja na Luseshelo Mwashilindi ambaye inadaiwa alikuwa ameyahifadhi nyumbanmi kwake mabaki ya mwili huo, ikiwa ni vipande vinne vikiwamo viwili vinavyosadikiwa kuwa ni sehemu ya mikono ya mabaki ya mwili huo. kweli ipo haja ya kuwachunguza hawa wachungaji wa makanisa ya leo, huyu anaechunga kondoo wa bwana anashiriki kuwapiga deal albino, kinachokera wakati wanatafuta wateja eti wakawa wananadi kuwa wanauza viungo vya kunguru mweupe.

No comments:

Post a Comment