Mwene Mkuu, Masoko, alimwambia Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, kuwa wao wanakamati zao za ufundi na kama serikali ikiwapa kibali watawashughulikia wanaume wanaowajaza mimba wanafunzi kwa kuwahamishia katika matumbo yao na wanafunzi kuendelea na masomo kama kawaida, "yaani ipo hivi wewe, kwa mfano Juma umejifanya kidume unampa mimba Vanesa ambaye ni mwanafunzi, sasa hawa machifu kupitia darubini zao wanakuona wewe ndio muhusika, na kwa kutumia kamati ya ufundi wanachukua hiyo mimba na kuiweka katika tumbo lako'
Lakini wazee wa mila hao wakasonga mbele zaidi na kusema wapiga nondo nao wakae tayari tayari kwa kuwa kupitia darubini zao watawaona na kuwatengua miguu, kuwafanya wajipeleke polisi na walio na viungo vya binadamu watajitokeza hadharani wakiwa wamevibeba na polisi kuwakamata kiulaini kama wananawa. Habri ndio hiyo tukae mkao wa kula tukisubiri kuona wanaume wakiwa na mimba na si vitambi tena.
No comments:
Post a Comment