Wednesday, March 11, 2009

Heshimaaaaa toa

Ni Vijana wakakamavu, lakini lipo jambo kidogo linasikitisha. Wakiwa kama watanzania wengine wenye ajira, askari wa kampuni binafsi za ulinzi ndio wanaolipwa kiduchu pengine kuliko hata house girl anayefanya kazi kwa kibosile.
Kwanza wanakesha wakilinda mali zenye thamani ya mamilioni ya shilingi, lakini hivi karibuni Chama cha makampuni ya ulinzi binafsi kilitangaza kuwa askari waliopo chini ya makampuni hayo watawajibika kuwalinda albino ili wasiendelee kuawa ingawa bado vitendo hivyo vya kinyama na kishenzi vinaendelea.
Sasa kuna swali huwa najiuliza, hawa walinzi wa sekta binafsi wengi wao mishahara yao ni kati shilingi 25,000 au 35,000 wanafamilia na watu wanaowategemea, kwa kuamua kuwalinda albino ni jambo jema sana,lakini nyie wamiliki hebu waongezeeni mishahara japo kidogo ili wasigeuka kuwa wezi katika maeneo wanayoyalinda.

No comments:

Post a Comment