Tuesday, March 10, 2009

Meli hii kuwa mali ya Tanzania?

Askari akilinda meli iliyokamatwa katika bahari ya hindi ikifanya shughuli za uvuvi haramu, hata hivyo meli hiyo haijulikani ni ya nchi gani huku mabaria karibu 30 waliokutwa ndani ya meli hiyo wakishindwa kuhojiwa kwa kile kilichodaiwa kuwa wanazungumza lugha ya ajabu na isiyo eleweka ni ya Taifa gani. ila jana kwenye TV niliwaona kama wakionyesha alama ya dole kwa wapiga picha wa tv.

Habari njema ni kuwa meli hiyo inaweza kuwa mali ya Tanzania ikiwa wamiliki wa meli hiyo watashindwa kulipa faini ya bilioni 20 ikiwa ni kosa la kuingia katika eneo la Tanzania kufanya shughuli za uvuvi haramu bila ya kuwa na vibali.

No comments:

Post a Comment