Tuesday, March 24, 2009

Tukumbuke kidogo hili

kwa mataifa ya wenzetu kiongozi wa Kitaifa kushambuliwa si jambo dogo, lakini kwa hili la kupigwa kwa Mzee Ruksa linapaswa kuangaliwa vizuri kidogo, ni kweli tunafahamu kuwa ugonjwa wa ukimwi upo na mtu anaweza kuupata ikiwa atafanya ngono isiyo salama na kuwa na wapenzi wengi kwelikweli. Ili kuzuia maambukizi mapya wataalami wakabuni kondomu ambayo inasaidia kupunguza maambukizi mapya ya vvu kwa maana isipotumiwa kwa usahihi bado unaweza kuupata ukimwi hata kama umevaa kondomu. Hoja yangu, hivi misimamo ya dini na mtu mmoja mmoja inapaswa kuchukuliwa kama ndio msimamo wa Watanzania, ambaye hataki kutumia kondomu ni lazima aonyeshe msimamo wake kwa vurugu? Kijana Said akipokea kichapo baada ya kumchapa kibao mzee Ruksa.

No comments:

Post a Comment