Monday, March 9, 2009

Biashara

Biashara ndogo ndio msingi wa maisha ya watanzania wengi hususani wanawake. ni biashara za machungwa, ndizi, mboga za majani na nyinginezo ambazo hata mtaji wake hauzidi shilingi 50,000,wengi wanaishi katika nyumba za kupanga huku wakiwa na familia zinazowategemea na wanasomesha watoto. Mikopo, Serikali na taasisi za fedha zimekuwa zikiwahamasisha wananchi kukopa ili waweze kuwa na miradi endelevu na inayoweza kuwainua kiuchumi, lakini riba za mikopo hiyo zimekuwa ni tishio na kusababisha wengi washindwe kukopa, pia wengi hawana vitu vya kuwekeza kama dhamana. Ipo haja kwa serikali kuweka mkakati utakaowasaidia watanzania wa kawaida kuwa na uwezo wa kupata mikopo.

No comments:

Post a Comment