Thursday, November 14, 2013

Kilimo cha kahawa



Zaidi ya Baiskeli 100 zenye thamani ya shilingi milioni 16.5 zimegawiwa kwa wakulima wa kahawa, wahamasishaji wa kilimo hifadhi pamoja na wakulima wawezeshaji  katika wilaya nne za Mkoa wa Mbeya zinazijihusisha na kilimo cha kahawa.

Meneja shughuli wa shirika la Hanns R. Neumann Stiftung Africa Ltd, Webster Miyanda alisema lengo la kugawa baiskeli hizo ni kuwawezesha wakulima na wahamasishaji wa kilimo hifadhi  kuweza kutekeleza majukumu yao ya kila siku ambapo wakulima waliofadika ni wa wilaya za Mbeya, Ileje, Rungwe na Mbozi.

Alisema wameamua kugawa baiskeli hizo kwa wakulima kwa kuwa wamebaini zinarahisha shughuli kwa wakulima  ambapo alisema hivi sasa wamehasika kuhudhuria mafunzo ya kilimo bora cha kahawa, ufuatiliaji wa mabadiliko ya tabia nchi kwa kuchukua jotoridi la kila siku na uboreshaji na uendelezaji wa kilimo hifadhi cha mahindi.

“Hii ni awamu ya pili, awali tulitoa baiskeli 100 na baada ya kuona kuwa kunamatokeo chanya kwa wakulima na wawezeshaji wa kilimo hifadhi tumeona tuongeze zingine na lengo letu ni kuhakikisha wakulima wote wanapata baiskeli ili waweze kufika kwenye  mikutano yao ya vijiji na kushiriki mafunzo kwa urahisi” alisema.
Aidha Miyanda alisema kabla ya kugawa baiskeli, wakulima walikuwa hawatekelezi miradi na mafunzo wanayokuwa wamepewa, “kwa mfano tulikuwa tunaandaa shamba darasa na kuwafundisha, tukiondoka hadi tunarudi hakuna linalokuwa limefanyika, hivyo tukagundua kwamba usafiri ni tatizo katika utekelezaji na tukaona tuanze kwa kuwapa baiskeli” alisema.
Kadhalika alisema upatikanaji wa baiskeli hizo umerahisha wahamasishaji na wawezeshaji kuweza kushirikiana kwa urahisi na kuweza kubadilishana taarifa na maafisa ugani hivyo kusaidia kuboresha shughuli za kilimo hivyo kumsaidia mkulima kuboresha kipato chake.

Kwa upande wake, muhamasishaji wa kilimo cha kahawa kutoka kijiji cha Igale, alisema kukosekana kwa mvua za uhakika kumeanza kuathiri shughuli za kilimo cha kahawa, ambapo alisema kuwa ili kukabiliana na tatizo hulo hivi sasa wameanza kuweka matandazo mashambani ili kuhifadhi unyevu unyevu kwenye miche ya kahawa.

Akizungumzia msaada wa baiskeli, alisema zimewasaidia katika kuharakisha utendaji wa shughuli za kila siku ambapo hivi sasa wanaweza kusafiri kutoka eneo moja hadi jingine bila ya kulazimika kutembea kwa mguu kama ilivyokuwa zamani jambo ambalo lilikuwa linakwamisha utekelezaji wa shughuli za maendeleo.

Shirika la Hanns R. Neumann Stiftunga Africa Ltf limekuwa likijihusha na utoaji wa elimu ya kilimo bora cha kahawa pamoja na kuwawezesha wakulima kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ambayo kwa kiasi kikubwa yanaathiri kilimo cha zao hilo.



No comments:

Post a Comment