Sunday, November 24, 2013

Dodoma kupitia Mtera kwenda Mbeya

*Safari ya jasho, mateso na vilio kwa watoto.

Njia iliyozoeleka kwa wasafiri wanaotoka Mkoa wa Mbeya kwenda Makao Makuu ya nchi Mkoani Dodoma ni kupitia Mikoa Iringa, Morogoro na hatimaye Dodoma  ambapo safari ni takribani zaidi ya masaa 14 barabarani kwa maana unaondoka Mbeya saa 12 asubuhi na kufika      Dodoma kati ya saa 1 na saa 2 usiku.

Lakini ukapatikana ushauri kuwa unaporudi Mbeya, panda basi linalopita njia ya Makato kutoka Dodoma, Mtera, Iringa na Mbeya na kuwasili Mbeya majira ya saa 7 au 8 mchana





Kilichojiri sasa
Safari ilianza saa 12:00 asubuhi kama ilivyoandikwa kwenye tiketi, lakini baada ya hapo gari lilianza kupakia kila abiria waliokuwepo barabarani na kusababisha hali ya hewa ndani ya basi kubadilika na kuwa ya joto kali, vilio kwa watoto na mateso kwa abiria waliosimama na waliokaa huku wakiwa hawana hata nafasi ya kusimama wala kusogea.

Miundombinu ya barabara ni mizuri na kwa kiwango kikubwa barabara ni ya rami.Ipo haja kwa wamiliki wa vyombo vya usafirishaji abiria kuongeza magari katika barabara hiyo ili kuwasaidia wananchi wa maeneo hayo waweze kusafiri kwa usalama na amani tofauti na sasa  ambapo usafiri ni wa mashaka na unaofanya abiria kujiuliza je tutafika na roho zetu?




 Abiria wakiwa wameminyana ndani ya basi kiasi cha kusababisha vilio kwa watoto kutokana na joto kal;i, kukosekana kwa hewa ya kutosha.(picha zote na Merali Chawe




 Usafiri huu wa basi, na idadi kubwa ya abiria waliojazana na kusababisha watu kukosa hewa safi,kuvuja jasho mithili ya mtu aliyetoka kuoga, ukanikumbusha wafungwa waliokufa wilayani Mbarali kutokana kukosa hewa.





Licha ya kukosa hewa wasafiri wanakuwa katika hatari kubwa ya kupata magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya hewa kama kifua kikuu, kikohozi na mangine ambayo kwa njia moja ama nyingine yanasababisha waathirika kushindwa kushiriki katika shughuli za kiuchumi

Dodoma kwenda Mbeya kupitia Mtera ni njia nzuri na fupi wamiliki wa magari ya biashara pelekeni magari yenu, lakini yawe yenye kiwango na sio mabovu.

No comments:

Post a Comment