Tuesday, February 18, 2020

JIANG

TSN new year party ya mwisho, Jan 2006. Photo point studio siku nyingi. photographed by mwenye blog ya dodoma.
kwenye futari ya marehemu amina chifupa
ofisini

Wednesday, February 12, 2014

Wasomi watakiwa kutotumia jazba kujadili masuala ya muungano

Na Merali Chawe, Mbeya

Wasomi nchini wametakiwa kujadili hoja za muungano kwa umakini na busara na waepuke jazba ambazo hazina maslahi kwa Taifa.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro aliyasema hayo alipokuwa akifungua Kongamano la wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu vilivyopo Mkoani hapa lillojadili tathmini ya miaka 50 ya utekelezaji wa masuala ya Muungano.

Alisema wasomi wanatakiwa kujadili hoja za Muungano kwa kuwa makini, wastahmilivu na wawe makini kutoa maoni kwa manufaa makubwa na mustakabali wa Taifa.
Na Merali Chawe , Mbeya

Baadhi ya wakazi Mkoani Mbeya wameuomba uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kuwajengea jengo la kupumzikia wakati wakisubiri kuwaona wagonjwa wao ili kuepuka adha za mvua na jua kali.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, walisema kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakilazimika kukaa kwenye jua na wakati mwingine kunyeshewa na mvua wakati wakisubiri muda wa kuruhusiwa kuinia kuona wagonjwa wao.

Thursday, December 19, 2013

Elimu

Kukosa kuungwa mkono na wazazi, walezi pamoja na kuamini kuwa kunahitajika nguvu kubwa katika utendaji wa kazi imedaiwa kuwa chanzo cha wasichana kukimbia masomo ya sayansi na uhandisi.

Hayo yalisemwa na baadhi ya washiriki wa mafunzo ya mafundi wa majokofu na viyoyozi kuhusu teknolojia mbadala za upozaji rafiki kwa tabaka la Ozoni yanayofanyika katika Hoteli ya Paradise Jijini Mbeya.

Mkufunzi kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia (Must), Moses Malole alisema kuwa imani kuwa kazi za uhandisi zinahitaji matumizi ya nguvu pamoja na kutoungwa mkono na wazazi imekuwa ni kichochea cha idadi kubwa ya wasichana kuyaepuka masomo ya uhandisi na sayansi.

Wednesday, December 18, 2013

Kilimo

Wakulima wilayani Chunya wameingiza shilingi bilioni 90 katika msimu wa kilimo uliopita kutokana na mauzo ya mazao ya ufuta,karanga, alizeti na tumbaku.
Mkuu wa wilaya ya Chunya, Deodatus Kinawilo aliyasema hayo alipokuwa akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo ya kuvijengea uwezo vikundi vya wakulima wa zao la alizeti wilayani humo.
Alisema kuwa kutokana na mapato hayo inadhihirisha kuwa shughuli za kilimo zinamanyfaa kiuchumi kutokana na wakulima kuweza kupata shilingi bilioni tisini katika msimu mmoja wa kilimo ambapo alisema kuwa wananchi wanatakiwa kuacha kulalamikia ugumu wa maisha na badala yake wafanye kazi.
Akitoa mchanganuo wa mapato hayo, Kinawilo alisema wakulima wa alizeti walipata shilingi bilioni nne, ufuta bilioni 27, karanga bilioni 12 na tumbaku bilioni 47, hata hivyo alisema licha ya mapato hayo eneo linalolimwa ni dogo ikilinganishwa na eneo linalofaa kwa kilimo.

Wednesday, December 11, 2013

Michezo


 Hatimaye baada ya hadithi za muda mrefu na shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) kuufungia uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine Mbeya, iwanja huo umeanza kufanyiwa ukarabati katika eneo la kuchezea (pitch) ili uweze kuwa kwenye kiwango na kuweza kutumika kwa michuano mbalimbali ya mpira wa miguu.

Meneja wa Uwanja huo, Modestus Mwaluka anasema tatizo la uwanja huo sio kubwa sana na ukarabati wake utakuwa ni wa muda mfupi na uwanja utakuwa tayari kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi kuu ya vodacom.

 Picha ya juu na chini zikionyesha ukarabati unaoendelea katika uwanja huo ambao unatumiwa na timu ya Tanzania Prisons na Mbeya City kama uwanja wa nyumbani. Mara kadhaa uwanja huo umekuwa ukilalamikiwa hasa na timu za Yanga na Simba kuwa ni mbovu na haufai hasa katika nyakati ambazo zinashindwa kuibuka na ushindi na zikishinda uwanja huwa unakuwa ni mzuri.


Hata hivyo pamoja na ukarabati wa sehemu ya kuchezea bado wamiliki wa uwanja huo wanakabiliwa na changamoto ya kuhakikisha uwanja huo unakuwa katika hali ya usafi na kuboresha mazingira katika nyakati zote ikiwemo kujenga vyoo vipya kwa ajili ya mashabiki wa soka na wananchi wanaofika uwanjani hapo kwa shughuli mbalimbali.

Thursday, December 5, 2013

Kweli tatizo la vijana sio siasa

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana amesema kuwa tatizo la vijana nchini si siasa na vyama vya siasa kama CCM, Chadema au NCCR Mageuzi na kwamba tatizo lao kubwa ni ukosefu wa ajira.

Kinana aliyasema hayo jana wakati akifuhutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Jijini Mbeya ambapo alisema kuwa vijana wamekuwa wakijihusisha na maandano ya kisiasa wakiamini wanaweza wakapata chochote.

Alisema kuwa ili kuwawezesha vijana kujiajiri ipo haja kwa serikali kufufua viwanda vilivyokufa, hata hivyo alisema kuwa serikali haiwezi kuajiri watanzania wote bali inatakiwa kutengeneza mazingira yatakayowawezesha vijana kujiajiri.

Wednesday, December 4, 2013

Hatari kwa afya

Mtoto akichota maji machafu katika dimbwi la Maji, ni muhimu kwa wazazi kuwa makini kwa kuwaangalia watoto michezo wanayocheza na vitu wamavyochezea ili kuhakikisha wanakuwa na afya nje na hawapati magonjwa ya kuambukiza ambauo ni hatari kwa afya zao.

Thursday, November 28, 2013


Watoto wakisakata kabumbu huku wakiwa pekupeku na mpira wa makaratasi maarufu kama kinyenga, vipaji vingi vya watoto vimekuwa vikipotelea mtaani kutokana na kukosekana kwa mfumo bora wa kuendeleza vipaji vya watoto.

Wednesday, November 27, 2013

 Wafanyabiashara wa matikiti maji wakisubiria wateja wanaosafiri kutoka Dodoma ili wawauzie bidhaa zao na wao kupata fedha za kujikimu na kuendeleza biashara zao ndogo.

Mandhari ya milima ya kueleka Iringa kutokea Mtera, ni milima yenye mandhari ya kuvutia na ujenzi wa kiwango cha lami ukiwa unaendelea. Kuboreshwa kwa miundo mbinu ya barabara kunasaidia kuboresha na kurahisisha usafiri wa kutoka eneo moja kwenda lingine na hivyo kuharakisha shughuli za maendeleo