Yangu Macho
Kupitia blog hii utapata nafasi ya kuyajua mambo yanayojiri kila siku katika Mkoa wa Mbeya zikiwemo, habari mbalimbali zinazohusu jamii, matukio, na tetesi mbalimbali. Pia kupitia blog hii tutajadili masuala mbalimbali ya maendeleo yanayohusu Mkoa wa Mbeya.
Tuesday, February 18, 2020
Wednesday, February 12, 2014
Wasomi watakiwa kutotumia jazba kujadili masuala ya muungano
Na Merali Chawe, Mbeya
Wasomi nchini wametakiwa kujadili hoja za muungano kwa umakini na busara na waepuke jazba ambazo hazina maslahi kwa Taifa.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro aliyasema hayo alipokuwa akifungua Kongamano la wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu vilivyopo Mkoani hapa lillojadili tathmini ya miaka 50 ya utekelezaji wa masuala ya Muungano.
Alisema wasomi wanatakiwa kujadili hoja za Muungano kwa kuwa makini, wastahmilivu na wawe makini kutoa maoni kwa manufaa makubwa na mustakabali wa Taifa.
Wasomi nchini wametakiwa kujadili hoja za muungano kwa umakini na busara na waepuke jazba ambazo hazina maslahi kwa Taifa.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro aliyasema hayo alipokuwa akifungua Kongamano la wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu vilivyopo Mkoani hapa lillojadili tathmini ya miaka 50 ya utekelezaji wa masuala ya Muungano.
Alisema wasomi wanatakiwa kujadili hoja za Muungano kwa kuwa makini, wastahmilivu na wawe makini kutoa maoni kwa manufaa makubwa na mustakabali wa Taifa.
Na Merali Chawe , Mbeya
Baadhi ya wakazi Mkoani Mbeya wameuomba uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kuwajengea jengo la kupumzikia wakati wakisubiri kuwaona wagonjwa wao ili kuepuka adha za mvua na jua kali.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, walisema kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakilazimika kukaa kwenye jua na wakati mwingine kunyeshewa na mvua wakati wakisubiri muda wa kuruhusiwa kuinia kuona wagonjwa wao.
Baadhi ya wakazi Mkoani Mbeya wameuomba uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kuwajengea jengo la kupumzikia wakati wakisubiri kuwaona wagonjwa wao ili kuepuka adha za mvua na jua kali.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, walisema kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakilazimika kukaa kwenye jua na wakati mwingine kunyeshewa na mvua wakati wakisubiri muda wa kuruhusiwa kuinia kuona wagonjwa wao.
Thursday, December 19, 2013
Elimu
Kukosa kuungwa mkono na wazazi, walezi pamoja na
kuamini kuwa kunahitajika nguvu kubwa katika utendaji wa kazi imedaiwa kuwa
chanzo cha wasichana kukimbia masomo ya sayansi na uhandisi.
Hayo yalisemwa na baadhi ya washiriki wa mafunzo ya
mafundi wa majokofu na viyoyozi kuhusu teknolojia mbadala za upozaji rafiki kwa
tabaka la Ozoni yanayofanyika katika Hoteli ya Paradise Jijini Mbeya.
Mkufunzi kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia
(Must), Moses Malole alisema kuwa imani kuwa kazi za uhandisi zinahitaji
matumizi ya nguvu pamoja na kutoungwa mkono na wazazi imekuwa ni kichochea cha
idadi kubwa ya wasichana kuyaepuka masomo ya uhandisi na sayansi.
Wednesday, December 18, 2013
Kilimo
Wakulima wilayani Chunya wameingiza shilingi bilioni 90
katika msimu wa kilimo uliopita kutokana na mauzo ya mazao ya ufuta,karanga,
alizeti na tumbaku.
Mkuu wa wilaya ya Chunya, Deodatus Kinawilo aliyasema
hayo alipokuwa akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo ya kuvijengea uwezo
vikundi vya wakulima wa zao la alizeti wilayani humo.
Alisema kuwa kutokana na mapato hayo inadhihirisha kuwa
shughuli za kilimo zinamanyfaa kiuchumi kutokana na wakulima kuweza kupata
shilingi bilioni tisini katika msimu mmoja wa kilimo ambapo alisema kuwa
wananchi wanatakiwa kuacha kulalamikia ugumu wa maisha na badala yake wafanye
kazi.
Akitoa mchanganuo wa mapato hayo, Kinawilo alisema
wakulima wa alizeti walipata shilingi bilioni nne, ufuta bilioni 27, karanga bilioni
12 na tumbaku bilioni 47, hata hivyo alisema licha ya mapato hayo eneo
linalolimwa ni dogo ikilinganishwa na eneo linalofaa kwa kilimo.
Wednesday, December 11, 2013
Michezo
Hatimaye baada ya hadithi za muda mrefu na shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) kuufungia uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine Mbeya, iwanja huo umeanza kufanyiwa ukarabati katika eneo la kuchezea (pitch) ili uweze kuwa kwenye kiwango na kuweza kutumika kwa michuano mbalimbali ya mpira wa miguu.
Meneja wa Uwanja huo, Modestus Mwaluka anasema tatizo la uwanja huo sio kubwa sana na ukarabati wake utakuwa ni wa muda mfupi na uwanja utakuwa tayari kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi kuu ya vodacom.
Picha ya juu na chini zikionyesha ukarabati unaoendelea katika uwanja huo ambao unatumiwa na timu ya Tanzania Prisons na Mbeya City kama uwanja wa nyumbani. Mara kadhaa uwanja huo umekuwa ukilalamikiwa hasa na timu za Yanga na Simba kuwa ni mbovu na haufai hasa katika nyakati ambazo zinashindwa kuibuka na ushindi na zikishinda uwanja huwa unakuwa ni mzuri.
Hata hivyo pamoja na ukarabati wa sehemu ya kuchezea bado wamiliki wa uwanja huo wanakabiliwa na changamoto ya kuhakikisha uwanja huo unakuwa katika hali ya usafi na kuboresha mazingira katika nyakati zote ikiwemo kujenga vyoo vipya kwa ajili ya mashabiki wa soka na wananchi wanaofika uwanjani hapo kwa shughuli mbalimbali.
Thursday, December 5, 2013
Kweli tatizo la vijana sio siasa
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana amesema kuwa tatizo la vijana nchini si siasa na vyama vya siasa kama CCM, Chadema au NCCR Mageuzi na kwamba tatizo lao kubwa ni ukosefu wa ajira.
Kinana aliyasema hayo jana wakati akifuhutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Jijini Mbeya ambapo alisema kuwa vijana wamekuwa wakijihusisha na maandano ya kisiasa wakiamini wanaweza wakapata chochote.
Alisema kuwa ili kuwawezesha vijana kujiajiri ipo haja kwa serikali kufufua viwanda vilivyokufa, hata hivyo alisema kuwa serikali haiwezi kuajiri watanzania wote bali inatakiwa kutengeneza mazingira yatakayowawezesha vijana kujiajiri.
Kinana aliyasema hayo jana wakati akifuhutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Jijini Mbeya ambapo alisema kuwa vijana wamekuwa wakijihusisha na maandano ya kisiasa wakiamini wanaweza wakapata chochote.
Alisema kuwa ili kuwawezesha vijana kujiajiri ipo haja kwa serikali kufufua viwanda vilivyokufa, hata hivyo alisema kuwa serikali haiwezi kuajiri watanzania wote bali inatakiwa kutengeneza mazingira yatakayowawezesha vijana kujiajiri.
Wednesday, December 4, 2013
Hatari kwa afya
Mtoto akichota maji machafu katika dimbwi la Maji, ni muhimu kwa wazazi kuwa makini kwa kuwaangalia watoto michezo wanayocheza na vitu wamavyochezea ili kuhakikisha wanakuwa na afya nje na hawapati magonjwa ya kuambukiza ambauo ni hatari kwa afya zao.
Thursday, November 28, 2013
Wednesday, November 27, 2013
Wafanyabiashara wa matikiti maji wakisubiria wateja wanaosafiri kutoka Dodoma ili wawauzie bidhaa zao na wao kupata fedha za kujikimu na kuendeleza biashara zao ndogo.
Mandhari ya milima ya kueleka Iringa kutokea Mtera, ni milima yenye mandhari ya kuvutia na ujenzi wa kiwango cha lami ukiwa unaendelea. Kuboreshwa kwa miundo mbinu ya barabara kunasaidia kuboresha na kurahisisha usafiri wa kutoka eneo moja kwenda lingine na hivyo kuharakisha shughuli za maendeleo
Mandhari ya milima ya kueleka Iringa kutokea Mtera, ni milima yenye mandhari ya kuvutia na ujenzi wa kiwango cha lami ukiwa unaendelea. Kuboreshwa kwa miundo mbinu ya barabara kunasaidia kuboresha na kurahisisha usafiri wa kutoka eneo moja kwenda lingine na hivyo kuharakisha shughuli za maendeleo
Subscribe to:
Posts (Atom)