Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana amesema kuwa tatizo la vijana nchini si siasa na vyama vya siasa kama CCM, Chadema au NCCR Mageuzi na kwamba tatizo lao kubwa ni ukosefu wa ajira.
Kinana aliyasema hayo jana wakati akifuhutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya Ruanda Nzovwe Jijini Mbeya ambapo alisema kuwa vijana wamekuwa wakijihusisha na maandano ya kisiasa wakiamini wanaweza wakapata chochote.
Alisema kuwa ili kuwawezesha vijana kujiajiri ipo haja kwa serikali kufufua viwanda vilivyokufa, hata hivyo alisema kuwa serikali haiwezi kuajiri watanzania wote bali inatakiwa kutengeneza mazingira yatakayowawezesha vijana kujiajiri.
No comments:
Post a Comment