Watoto wakisakata kabumbu huku wakiwa pekupeku na mpira wa makaratasi maarufu kama kinyenga, vipaji vingi vya watoto vimekuwa vikipotelea mtaani kutokana na kukosekana kwa mfumo bora wa kuendeleza vipaji vya watoto.
Kupitia blog hii utapata nafasi ya kuyajua mambo yanayojiri kila siku katika Mkoa wa Mbeya zikiwemo, habari mbalimbali zinazohusu jamii, matukio, na tetesi mbalimbali. Pia kupitia blog hii tutajadili masuala mbalimbali ya maendeleo yanayohusu Mkoa wa Mbeya.
Thursday, November 28, 2013
Wednesday, November 27, 2013
Wafanyabiashara wa matikiti maji wakisubiria wateja wanaosafiri kutoka Dodoma ili wawauzie bidhaa zao na wao kupata fedha za kujikimu na kuendeleza biashara zao ndogo.
Mandhari ya milima ya kueleka Iringa kutokea Mtera, ni milima yenye mandhari ya kuvutia na ujenzi wa kiwango cha lami ukiwa unaendelea. Kuboreshwa kwa miundo mbinu ya barabara kunasaidia kuboresha na kurahisisha usafiri wa kutoka eneo moja kwenda lingine na hivyo kuharakisha shughuli za maendeleo
Mandhari ya milima ya kueleka Iringa kutokea Mtera, ni milima yenye mandhari ya kuvutia na ujenzi wa kiwango cha lami ukiwa unaendelea. Kuboreshwa kwa miundo mbinu ya barabara kunasaidia kuboresha na kurahisisha usafiri wa kutoka eneo moja kwenda lingine na hivyo kuharakisha shughuli za maendeleo
Tuesday, November 26, 2013
Mandhari ya maeneo ya mtera, unaposafiri kutoka Dodoma kuelekea Mkoani Iringa au Mbeya, ipo haja ya kutunza mazingira ili kuendelea kuwa na maeneo ya kuvutia nchini.
Unaposafiri na basi ya Dodoma Mbeya kupitia Mtera abiria kujazana kupita kiasi huku wengine wakiwa wamebeba kuku ni jambo la kawaida kabisa, ipo haja kwa wataalamu wa afya kueleza athari za watu kujazana kupita kiasi katika vyombo vya usafiri huku wakiwa wamebeba mifugo
Unaposafiri na basi ya Dodoma Mbeya kupitia Mtera abiria kujazana kupita kiasi huku wengine wakiwa wamebeba kuku ni jambo la kawaida kabisa, ipo haja kwa wataalamu wa afya kueleza athari za watu kujazana kupita kiasi katika vyombo vya usafiri huku wakiwa wamebeba mifugo
Dk. Mwakyembe kufungua maonyesho ya kimataifa ya biashara
Waziri wa uchukuzi, Dk. harrison Mwakyembo leo anatarajia kuzindua maonyesho ya kimataifa ya biashara yatakayofanyika kwa wiki moja katika viwanja vya ukumbi wa mikutano wa mkapa uliopo Jijini Mbeya.
Maonyesho hayo yanatarajia kushirikisha makampuni kutoka nje ya nchini yakiwemo kutoka nchini Kenya na makapuni ya ndani ya nchi ambapo hadi kufikia jana maandalizi yalikuwa yamekamilika kwa zaidi ya asilimia 90 kwa washiriki kupanga bidhaa zao.
Sunday, November 24, 2013
Dodoma kupitia Mtera kwenda Mbeya
*Safari ya jasho, mateso na vilio kwa watoto.
Njia
iliyozoeleka kwa wasafiri wanaotoka Mkoa wa Mbeya kwenda Makao Makuu ya nchi
Mkoani Dodoma ni kupitia Mikoa Iringa, Morogoro na hatimaye Dodoma ambapo safari ni takribani zaidi ya masaa 14
barabarani kwa maana unaondoka Mbeya saa 12 asubuhi na kufika Dodoma kati ya
saa 1 na saa 2 usiku.
Friday, November 15, 2013
Thursday, November 14, 2013
Kilimo cha kahawa
Zaidi ya Baiskeli
100 zenye thamani ya shilingi milioni 16.5 zimegawiwa kwa wakulima wa kahawa,
wahamasishaji wa kilimo hifadhi pamoja na wakulima wawezeshaji katika
wilaya nne za Mkoa wa Mbeya zinazijihusisha na kilimo cha kahawa.
Meneja shughuli
wa shirika la Hanns R. Neumann Stiftung Africa Ltd, Webster Miyanda alisema
lengo la kugawa baiskeli hizo ni kuwawezesha wakulima na wahamasishaji wa
kilimo hifadhi kuweza kutekeleza majukumu yao ya kila siku ambapo
wakulima waliofadika ni wa wilaya za Mbeya, Ileje, Rungwe na Mbozi.
Subscribe to:
Posts (Atom)