Thursday, November 28, 2013


Watoto wakisakata kabumbu huku wakiwa pekupeku na mpira wa makaratasi maarufu kama kinyenga, vipaji vingi vya watoto vimekuwa vikipotelea mtaani kutokana na kukosekana kwa mfumo bora wa kuendeleza vipaji vya watoto.

Wednesday, November 27, 2013

 Wafanyabiashara wa matikiti maji wakisubiria wateja wanaosafiri kutoka Dodoma ili wawauzie bidhaa zao na wao kupata fedha za kujikimu na kuendeleza biashara zao ndogo.

Mandhari ya milima ya kueleka Iringa kutokea Mtera, ni milima yenye mandhari ya kuvutia na ujenzi wa kiwango cha lami ukiwa unaendelea. Kuboreshwa kwa miundo mbinu ya barabara kunasaidia kuboresha na kurahisisha usafiri wa kutoka eneo moja kwenda lingine na hivyo kuharakisha shughuli za maendeleo

Tuesday, November 26, 2013

Wakinamama wafanyabiashara ndogo wakiwaonyesha bidhaa abiria (hawapo pichani) waliokuwa wakisafiri kati ya Dodoma, Mtera, Iringa na Mbeya, licha ya uchumi mdogo biashara ndogo zimekuwa zikiwawezesha wanawake kumudu kuhudumia familia na kusomesha watoto wao kwa mafanikio.

     Mandhari ya maeneo ya mtera, unaposafiri kutoka Dodoma kuelekea Mkoani Iringa au Mbeya, ipo haja ya kutunza mazingira ili kuendelea kuwa na maeneo ya kuvutia nchini.

Unaposafiri na basi ya Dodoma Mbeya kupitia Mtera abiria kujazana kupita kiasi huku wengine wakiwa wamebeba kuku ni jambo la kawaida kabisa, ipo haja kwa wataalamu wa afya kueleza athari za watu kujazana kupita kiasi katika vyombo vya usafiri huku wakiwa wamebeba mifugo
Dk. Mwakyembe kufungua maonyesho ya kimataifa ya biashara
 
Waziri wa uchukuzi, Dk. harrison Mwakyembo leo anatarajia kuzindua maonyesho ya kimataifa ya biashara yatakayofanyika kwa wiki moja katika viwanja vya ukumbi wa mikutano wa mkapa uliopo Jijini Mbeya.
 
Maonyesho hayo yanatarajia kushirikisha makampuni kutoka nje ya nchini yakiwemo kutoka nchini Kenya na makapuni ya ndani ya nchi ambapo hadi kufikia jana maandalizi yalikuwa yamekamilika kwa zaidi ya asilimia 90 kwa washiriki kupanga bidhaa zao.

Sunday, November 24, 2013

Dodoma kupitia Mtera kwenda Mbeya

*Safari ya jasho, mateso na vilio kwa watoto.

Njia iliyozoeleka kwa wasafiri wanaotoka Mkoa wa Mbeya kwenda Makao Makuu ya nchi Mkoani Dodoma ni kupitia Mikoa Iringa, Morogoro na hatimaye Dodoma  ambapo safari ni takribani zaidi ya masaa 14 barabarani kwa maana unaondoka Mbeya saa 12 asubuhi na kufika      Dodoma kati ya saa 1 na saa 2 usiku.

Lakini ukapatikana ushauri kuwa unaporudi Mbeya, panda basi linalopita njia ya Makato kutoka Dodoma, Mtera, Iringa na Mbeya na kuwasili Mbeya majira ya saa 7 au 8 mchana

Friday, November 15, 2013

Eti Mwanafunzi wa chuo cha Ualimu uyole, aliyetajwa kwa jina moja la Joseph anadaiwa kukutwa akiwa amejinyonga katika mto nzovwe uliopo Jijini Mbeya.marehemu alikuwa anachukua degree mwaka wa kwanza, sababu ya kujinyonga haijajulikana, mwili wa marehemu upo rufaa

Thursday, November 14, 2013

Kilimo cha kahawa



Zaidi ya Baiskeli 100 zenye thamani ya shilingi milioni 16.5 zimegawiwa kwa wakulima wa kahawa, wahamasishaji wa kilimo hifadhi pamoja na wakulima wawezeshaji  katika wilaya nne za Mkoa wa Mbeya zinazijihusisha na kilimo cha kahawa.

Meneja shughuli wa shirika la Hanns R. Neumann Stiftung Africa Ltd, Webster Miyanda alisema lengo la kugawa baiskeli hizo ni kuwawezesha wakulima na wahamasishaji wa kilimo hifadhi  kuweza kutekeleza majukumu yao ya kila siku ambapo wakulima waliofadika ni wa wilaya za Mbeya, Ileje, Rungwe na Mbozi.