Kukosa kuungwa mkono na wazazi, walezi pamoja na
kuamini kuwa kunahitajika nguvu kubwa katika utendaji wa kazi imedaiwa kuwa
chanzo cha wasichana kukimbia masomo ya sayansi na uhandisi.
Hayo yalisemwa na baadhi ya washiriki wa mafunzo ya
mafundi wa majokofu na viyoyozi kuhusu teknolojia mbadala za upozaji rafiki kwa
tabaka la Ozoni yanayofanyika katika Hoteli ya Paradise Jijini Mbeya.
Mkufunzi kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia
(Must), Moses Malole alisema kuwa imani kuwa kazi za uhandisi zinahitaji
matumizi ya nguvu pamoja na kutoungwa mkono na wazazi imekuwa ni kichochea cha
idadi kubwa ya wasichana kuyaepuka masomo ya uhandisi na sayansi.