Wednesday, January 28, 2009

Wananchi kususia uchaguzi Mbeya, kunani?

Picha ya Juu: Makamu Mwenyekiti Mstaafu, John Malecela akimnadi mchungaji Mwanjale
wakati wa kampeni
Picha ya Chini: Aliyekuwa mgombea wa Chadema, Mwanasheria Sambwee Shitambala, wa pili
kulia akiwa na mashabiki wa Chadema waliomsindikiza kurudisha na hatimaye
kuenguliwa
Januari 25, wananchi wa jimbo la Mbeya Vijijini walipiga kura kwa ajili ya kumchagua mbunge wao atakayemrithi aliyekuwa mbunge wa Jimbo hilo Richard Nyaulawa aliyefariki Novemba 9, mwaka jana kwa ugonjwa wa saratani ya utumbo.
Mchungaji wa Kanisa la Uinjilisti, Luckson Mwanjale ndiye aliyefanikiwa kuibuka kidedea na kumbwaga vibaya mgombea wa CUF, Daud Mponzi ambaye kitaaluma na Mhandisi na Mwanamama mfanyabiashara Subi Mwakipiki. Lakini ushindi huo wa CCM umeachwa maswali zaidi kuliko fura.
Waliojiandikisha kupiga kura walikuwa ni Watanzania 127,780, waliopiga kura ni 44,855 wananchi 82,925 hawakupiga kura hali ambayo inadaiwa kusababishwa Chadema kuenguliwa katika uchaguzi huo na ukosefu wa elimu ya demokrasia.
Watanzania wenzangu, tunamaoni gani katika hili.

No comments:

Post a Comment