Tuesday, January 27, 2009

Vijana

Ili uchumi wa Taifa lolote uweze kukua kwa kasi inahitajika nguvu kazi ya vijana ambayo ikiwa ikitumiwa kwa usahihi inaweza kuleta mabadiliko na kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kukuza uchumi wa nchi kwa kupitia sekta rasmi na isiyo rasmi.
Lakini kwa Tanzania, licha ya kuwa na rasimali nyingi pamoja na vijana wenye nguvu, ukosefu wa mitaji, vijana kutowezeshwa wengi wameishia kuwa wamachinga, kutembea na soksi mbili siku nzima akitafuta wateja na wengine kuishia kujiajiri kwa kuuza ndizi za kuchoma. Je watawala wetu wanania ya dhati ya kuwakomboa vijana?

No comments:

Post a Comment