Kupitia blog hii utapata nafasi ya kuyajua mambo yanayojiri kila siku katika Mkoa wa Mbeya zikiwemo, habari mbalimbali zinazohusu jamii, matukio, na tetesi mbalimbali. Pia kupitia blog hii tutajadili masuala mbalimbali ya maendeleo yanayohusu Mkoa wa Mbeya.
Friday, August 7, 2009
aaaaa Ludewa
Hivi karibuni nilibahatika kutembelea wilaya ya Ludewa Mkoani Iringa hii ikiwa ni mara yangu ya kwanza kabisa na hasa kufika Manda kandokando ya ziwa nyasa, yapo mengi niliyojifunza na mengine si ya kujivunia hata kidogo.
Cha kwanza ukiwasili Ludewa mjini na jioni wakati ukiwa unapata chakula au kinywaji kidogo si ajabu kufuatwa na msichana akaomba umnunulie soda na kuuliza umefikia wapi (akimaanisha guest), akiona unachelewa kumjibu pengine kwa kupigwa butwaa, ataongeza na jingine, "nasikia baridi unataka kunikumbatia?" bila hofu.
Kwa sisi wageni tulishangaa lakini wenyeji wakatuambia aaa hiyo ni kawaida kabisa, sijui ukiwa wewe utafanyaje na ukizingatia na huu ugonjwa wa ukimwi.
Mengi utayapata katika picha.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment