Friday, April 17, 2009

Big Psalm abatizwa, ilikuwa Pasaka

Hapa ilikuwa ni siku ya Pasaka, ambapo Big Psalm alibatizwa rasmi na Padri Mapunda wa Kanisa la Anglikana usharika wa Isanga, ambapo baada ya ubatizo Psalm akiwa na kundi lukuki la wajukuu wa Mzee Mng'ong'o walikwenda nyumbani kwa ajili ya shughuli za sherehe, anbapo siku hiyo watoto wengine wawili akiwemo wa baba yake Mkubwa Big Psalm alibatizwa.
Big Psalm akifurahia burudani ya show ya muziki ilikuwa ikiporomoshwa na watoto na wageni waalikwa "show yenyewe utishuhudia hapo chini"
Big Psalm akipiga makofi baada ya kufurahishwa na burudani iliyokuwa ikiporomoshwa na wacheza shoo "utawaona chini", hapa kilichomfurahisha ni wimbo wa jipange sawa sawa.
Big Psalm akifurahia jambo,
Big Psalm akijishika kichwa baada ya kukumbuka kuwa amesahau jambo la muhimu sana, wote tulipigwa na butwaa na kujiuliza ana nini.
Kumbe alisahau kupiga simu ya muhimu, hapa alikuwa tayari amenyang'anya simu ya Baba yake na kuwasiliana na mtu alikuwa anataka kumpigia, hakuna aliyejua ni nani huyo, mama watu wote muhimu walikuwepo.
Hapa akijadiliana jambo na mama yake mara baada ya kupiga simu hiyo.
Hapa Psalm kidogo ni kama alikuwa amezubaa huku mama yake akimtizama usoni, sijui walikuwa wamejibizana nini.
Hii ndiyo ile burudani uliyokuwa ukiisubiri kwa hamu, hapa wajomba na shangazi zake Psalm wakionyesha umahiri katika kusakata muziki wa injili,
Baba yake Mkubwa Psalm aliye kulia na Bibi yake mdogo hawakuwa nyuma katika kuonyesha ufundi wa kucheza nyimbo za injili kama wanavyoonekana picha ya juu na ya chini.
Hapa chini ni baadhi ya wageni waalikwa waliokuwa wakienda kutoa zawadi baada ya kupata burudani murua nyumbani kwa nyanya yake Psalm
Big Psalm bwana hata bado hajaondoka meza kuu tayari anataka kuanza kufungua zawadi na kubaini kilichomo ndani
Psalm vipi bwana, hapa alikuwa akiendelea na hekahela na kuhakikisha anafungua box la zawadi
Hapa uncle zake Pslam wakiwaaga nyanya zake Psalm ikiwa ni ishara ya kumaliza shughuli hiyo iliyokuwa ndogo lakini ilifana na kupendeza sana

1 comment: