Monday, October 5, 2009

Kombe la Duniani la Vijana wazururaji laja 2010

Kombe La Dunia La Vijana Wazururaji 2010:Tanzania Imo Tanzania ni miongoni mwa mataifa ambayo yatashirikishwa katika mashindano ya soka ya Kombe la Dunia, kwa vijana wanaozurura ovyo mitaani, yatakayofanyika mjini Durban, Afrika Kusini, mwezi Machi mwaka 2010. Mbali na wenyeji, mataifa mengine yatakayoshiriki ni Brazil, India, Nicaragua, Ufilipino, Ukraine, Uingereza na Vietman. Jumanne ya tarehe 22 Julai 2009, meneja wa chuo cha michezo cha watoto kutoka Mwanza,Tanzania, Bw Mutani Yangwe, alishiriki katika kikao mjini London kuzungumzia juu ya mashindano hayo ya dunia, na vile vile juu ya mipango ya Arsenal, klabu ya Uingereza, kukisaidia chuo hicho. SOURCE: BBC SWAHILI SERVICE.

Saturday, October 3, 2009

Kwa taarifa yako

Kwa tulio wengi lugha ya Kiingereza ni Tatizo, na tukifike kwenye mitumba tunababe nguo tu bila kuzingatia maana ya maneno yaliyomo kwenye fulana tunazovaa hebu soma maandishi katika fulana ya kijana na utakari ungekuwa wewe
unaweza usiamini lakini hii ndio Tanzania bwana na ndoto ya maisha bora kwa kila Mtanzania (source jamii forum)