Friday, September 25, 2009

Ludewa

natumai wote muwazima na mnaendelea vyema na shughuli za kila siku. Niwaombe radhi kwa kushindwa kuweka vitu vipya kila siku. Kuna mdau alivutiwa na picha za watoto wa Ludewa ambao walikuwa kipokea misaada ya nguo na baiskeli na akavutiwa na kuiona kuwa kuna haja ya yeye kwenda kutoa msaada kwa watoto hao. Ninachoweza kumshauri ni kuwasiliana moja kwa moja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ludewa, na kwa ushauri ikiwa mdau anahitaji kufika hadi manda aende kipindi cha kiangazi kwa kuwa mvua zikianza kwa mujibu wa wenyeji hakufikiki kwa urahisi. Asante